Loading...
Logo Zenevenes
Login
Logo Zenevenes
  • Home
  • Games

    • Logo Termo/Wordle Termo - Wordle 🇧🇷
    • Logo Termo/Wordle Colmeia - Spelling Bee 🇧🇷
  • Quotes
  1. Quotes
  2. Categorias
  3. imani
Voltar

Amri ya Kristo ilipima imani ya yule kipofu, ikiithibitisha na kuiimarisha. Bila kuchelewa au kusita, kipofu alitii amri ya Mungu: Alikwenda kuosha macho yake katika bwawa la Siloamu na aliona. Wengi wanaweza kuona ni kazi ya kipuuzi kwa mtu ambaye ni kipofu kufanya kazi ndogo kama hiyo ili aone. Lakini kwa vile alitii, kipofu alipona. Baraka huja kupitia utii. Kwa maana nyingine, kipofu alimtii Yesu bila kuona. Lakini matokeo yake, alipata kuona papohapo; ambapo baadaye, hatimaye, alipokea uponyaji halisi wa kiroho.

Enock Maregesi
faith blind amri-ya-kristo amri-ya-mungu bwawa-la-siloamu divine-decree imani kipofu the-command-of-christ utii

Vita ya Shetani na Mungu inatuathiri zaidi sisi wanadamu – na hapo baadaye itamuathiri Shetani pia. Vita hii haiwezi kuisha hadi siku ya mwisho, Yesu Kristo atakaporudi kuwachukua wateule wake. Pambana kwa njia ya maombi hadi siku ya mwisho kwa sababu adui tunayepambana naye hana muda wa kupumzika. Pambana kujiombea na kuwaombea wengine waliohai, na hata wale ambao bado hawajazaliwa, kabla mafuta ya dunia hii hayajalipuka. Usiishi kama adui wa msalaba wa Yesu Kristo, badala yake, ishi kama rafiki wa msalaba wa Yesu Kristo. Kuishi kama rafiki wa msalaba wa Yesu Kristo ni kupinga majivuno yote ya Shetani kwa upendo uliotukuka wa kujishusha au kujidharirisha, kutokutetereka hata kidogo na tamaa za ulimwengu huu kwa upendo mkubwa wa umaskini, na kutokuyumba wakati wa matatizo kwa sababu wakati wa amani ulijilimbikizia imani.

Enock Maregesi
love friend peace poverty faith pride god enemy fight humans jesus-christ needs battle satan prayers mungu adui imani amani day-of-judgement elects mafuta-ya-dunia-hii majivuno maombi matatizo msalaba-wa-yesu-kristo oil-of-this-world pambana rafiki shetani siku-ya-mwisho tamaa-za-ulimwengu-huu the-cross-of-jesus-christ the-desires-of-this-world umaskini upendo vita wanadamu wateule yesu-kristo

Pambana na Shetani kwa upanga wa imani ambao ni ukweli kwani ukweli ndiyo utakaokuweka huru.

Enock Maregesi
truth faith fight sword free satan imani pambana shetani huru ukweli upanga

Kumwamini Mwenyezi Mungu wakati wa raha ni rahisi kuliko kumwamini Mwenyezi Mungu wakati wa shida, na utahitaji imani kuendelea kumwamini wakati wa dhiki. Vipindi vigumu katika maisha yetu hutokea kwa kila mmoja wetu. Kuamini ya kwamba Mungu ana makusudi ya lazima kukuondolea vikwazo katika maisha yako ni vigumu sana wakati mwingine, lakini imani ndicho kitu cha muhimu zaidi unachotakiwa kuwa nacho katika kipindi hiki ambacho dunia imekata tamaa. Amani ya Mungu, ambayo huzidi hekima na maarifa yote ya kibinadamu, ni kuliamini neno la Mungu kwamba ni la kweli. Bila imani hutaweza kumfurahisha Mungu. Imani ni ufunguo wa nguvu, uwezo na neema ambavyo Mungu ametupangia. Kwa ufupi, Mungu ni mkubwa kuliko wewe na matatizo yako.

Enock Maregesi
life faith god power grace problems key ability comfort-zone difficulty obstacles mungu maisha imani matatizo amani-ya-mungu deliberately dhiki dunia-imekata-tamaa god-almighty makusudi mwenyezi-mungu neema nguvu peace-of-god ufunguo uwezo vikwazo wakati-wa-raha world-has-given-up

Kuna nguzo saba ambazo hazina budi kuzingatiwa kama unataka kuheshimiwa na kuwaheshimu wengine. Kwanza kabisa jitambue: wewe ni nani na unafanya nini hapa duniani. Halafu, kabla ya kusema jambo lolote kwa mtu yoyote fikiria kwanza maana au madhara ya hilo unalotaka kulisema. Kisha jifunze tamaduni mbalimbali na watendee wengine kama vile unavyotaka kutendewa au kama vile wanavyotaka kutendewa. Jifunze kusamehe na kusuluhisha migogoro katika jamii unamoishi huku ukidumisha heshima na utu kwa binadamu wenzako. Jijengee imani kwa watu, punguza upendeleo, fanya kazi kama timu kwani hakuna ‘mimi’ katika umoja ila kuna ‘sisi’, na jitahidi kwa kadiri ya uwezo wako WOTE kwa manufaa ya wote. Kuwa kiongozi katika kila jambo unalofanya na katika kila kitu unachofanya. Jitahidi kufanya jambo au kitu kwa usahihi kwa kadiri utakavyoweza.

Enock Maregesi
faith respect humanity society human i cultures unity leader know-yourself we all accuracy team conflicts mimi heshima imani binadamu favouritism jamii jitambue kiongozi kuheshimiwa migogoro sisi tamaduni timu to-be-respected umoja upendeleo usahihi utu wote

Kilio kikuu cha Yesu, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?”, yaani, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”, na “Imekwisha”, vilitabiriwa katika Zaburi 22 ili watu waliompinga Kristo waamini kama Yesu alikuwa Masihi. Zaburi 22 ulikuwa wimbo maarufu katika kipindi cha karne ya kwanza, kipindi ambacho Yesu alizaliwa na kufa, uliotungwa na mfalme Daudi, ulioitwa ‘zaburi ya mateso na matumaini ya mwadilifu’. Kwa hiyo Yesu aliposema maneno hayo yaliwaingia watu akilini, na kuanzia hapo imani hasa ya Ukristo ikachukua kasi hadi leo hii. Zaburi 22 inaanza na “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?” na inaisha na “Imekwisha”, miongoni mwa maneno saba aliyoyasema Yesu pale msalabani Golgotha. Kwa hiyo, Zaburi 22 ni utabiri wa kifo cha Yesu.

Enock Maregesi
faith song christianity christ jesus cross yesu messiah golgotha imani eloi-eloi-lama-sabakthani first-century imekwisha it-s-finished jesus-death karne-ya-kwanza kifo-cha-yesu king-david kristo maneno-saba masihi mfalme-daudi msalabani mungu-wangu my-god psalm-22 seven-words ukristo wimbo zaburi-22

Katika dunia ya leo ambapo mamilioni ya watu hutegemea utandawazi kupata pesa, kuwa na imani kwamba kupokea pesa kutoka kwa mtu usiyemjua au mtu mwenye nia mbaya na wewe ni kikwazo kikubwa cha maendeleo kwa sababu, karibu kila mtu unayekutana naye ni Shetani. Shetani ni mtu yoyote mwenye nia mbaya na wewe. Hivyo, kama uliwahi kuambiwa kwamba kupokea pesa kutoka kwa mtu usiyemjua ni kitu kibaya futa imani hiyo. Utaachaje kupokea pesa kutoka kwa mtu usiyemjua wakati kila siku unamwomba Mungu akusaidie, na Mungu hutenda kazi zake pale tunapojisahau? La sivyo hutapata pesa unayotamani kupata katika maisha yako, na kamwe hutawaamini watu. Zaka huondoa laana ya mapato. Toa zaka kununua pepo uliyopewa na Mungu.

Enock Maregesi
life faith god money development world satan paradise tithe mungu maisha malice globalization imani shetani curse-of-income dunia laana-ya-mapato maendeleo mamilioni-ya-watu millions-of-people mtu-usiyemjua nia-mbaya pepo pesa unanimous-person utandawazi zaka

Clique em "Aceitar" para armazenar Cookies que serão usados para melhorar sua experiência, análise de estatísticas de uso e nos ajudar a aperfeiçoar nossos serviços. Saiba mais

Ícone branco Zenevenes
Política de Privacidade | Termos de Uso
Zenevenes.com © 2025